SAUTI YA SHANGAZI YATOA TABASAMU KWA WANAFUNZI WA SHULE YA WASICHANA YA BUNGE


Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya Serikali ya Mwanamke kwa maendeleo endelevu (WSDO)  Bi Mary Mwenisongole, Alitembelea shule ya sekondari ya wasichana ya bunge kwa lengo la kutoa elimu ya kujitambua kwa wanafunzi hao ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa program ya SAUTI YA SHANGAZI yenye lengo la kutoa elimu ya kujitambua kwa Mabinti ikiwa na lengo la kuwakumbusha kuhusu safari yao ya mafanikio na uvaaji wa magauni matatu

Katika semina hiyo pamoja na mambo mengine ilitolewa elimu ya uzalendo, kujitambua, hedhi salama na dhana ya uvaaji wa magauni matatu kwa mtoto wa kike.   Aliwataka  wanafunzi kusoma kwa bidii, kumtanguliza Mungu mbele  na kutambua kuwa wao ni Taifa la Leo na kesho na kuyaishi malengo waliyojiwekea kwani inawezekana kuyafikia wakiamua

Pamoja na elimu hiyo waligawa mahitaji ya shule ikiwemo Mabegi ya shule, madaftari, Taulo za kike, Kalamu na Mpira kwa ajili ya michezo.


BINTI JITAMBUE, JIAMINI, JIKUBALI, UNAWEZA

Post a Comment

Previous Post Next Post