Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Maendeleo Endelevu (Hamburg Sustainability Conference) unaofanyika Hamburg Ujerumani ambao umefunguliwa rasmi na Chancellor wa Ujerumani Olaf Scholz leo terehe 07 October 2024. Kwenye mkutano huo, Mhe. Aweso ameandamana na Mhe. Hassani Iddi Mwamweta, Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani.
Mkutano huo umewakutanisha Marais, Mawaziri Wakuu, Rais wa Benki ya Dunia, Wakuu wa Taasisi za Kifedha kama IMF, Mawaziri, watu mashuhuri na Taasisi mbalimbali za maswala ya Maendeleo duniani.
Pamoja na mambo mengine. Mkutano huu unalenga kuwaleta pamoja wadau wote kutoka Sekta za Umma na binafsi kwa ajili ya kuunganisha nguvu ikiwemo upatikanaji wa Fedha ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endevu (SDGs).
Tags
Kimataifa