DKT MOLLEL AWAFARIJI WALIOUNGULIWA NA NYUMBA SIHA


Wananchi wa kata ya Ngarenairobi waliopata ajali ya kuunguliwa na nyumba zao wametakiwa kuwa watulivu  kwani  Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea  kuchunguza chanzo cha moto  na kuhakikisha  inawapatia huduma  muhimu  ili  kuendelea  na maisha yao  ya utafutaji. 

Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Siha (CCM) ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel alipofika katika kata ya Ngarenairobi  wilayani Siha mkoa  wa Kilimanjaro   na kuwafariji wahanga hao huku akiwahakikishia watoto  wao wanaendelea na masomo na huduma muhimu kwa wananchi zinaendelea kupatikana 

Dkt. Mollel  ametoa wito  huo  leo wakati  akielekea  katika  mkutano  wake na wananchi  wa kijiji  cha Roseline kata ya Ndumeti wilayani  humo ikiwa  ni  sehemu ya kuendeleza ziara yake Jimboni humo.

Post a Comment

Previous Post Next Post