Waziri wa Ghana akamatwa baada ya kashfa ya pesa taslimu $1m

 

Waziri wa zamani wa Usafi wa Mazingira na Rasilimali za Maji wa Ghana Cecilia Dapaah amekamatwa na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Maalum (OSP) baada ya kuripotiwa wizi wa $1m (£780,000) pesa taslimu kutoka kwa nyumba yake.

Kulingana na OSP, waziri huyo wa zamani aliwekwa chini ya kifungo cha nyumbani siku ya Jumapili tarehe 22 Julai kwa "makosa yanayoshukiwa ya rushwa na ufisadi".

Raia wengi wa Ghana na wanaharakati wa kupinga ufisadi wamehoji ni vipi mtumishi wa umma anaweza kuwa na pesa nyingi hivyo kufichwa nyumbani kwao huku kukiwa na mzozo wa kiuchumi nchini Ghana.

"Bi Dapaah anahojiwa na Maafisa walioidhinishwa wa OSP," taarifa hiyo ilisema

Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo alikubali kujiuzulu kwake Jumamosi kufuatia malalamiko ya umma.

Pesa hizo zilifichuliwa baada ya wafanyakazi wake wawili wa nyumbani kushtakiwa kwa kuiba pesa taslimu $1m, pamoja na €300,000 na cedi milioni kadhaa za Ghana, pamoja na baadhi ya vitu vya kibinafsi.

"Ninaweza kusema kwa msisitizo kwamba takwimu hizo haziwakilishi kwa usahihi kile ambacho mimi na mume wangu tuliripoti kwa polisi, ninafahamu sana kuhusu uzito wa hadithi kama hizo karibu na mtu katika nafasi yangu," Bi Dapaah alisema.

"Nina nia ya kushirikiana kikamilifu na mashirika yote ya serikali ili kuwawezesha kubaini ukweli kikamilifu," aliongeza.


Post a Comment

Previous Post Next Post