Kikao hiki kimejadili kiundani na kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma ya maji kwa ubora na kuhakikisha changamoto zote zinafanyiwa kazi.
Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Kata ya Kemondo imejenga mradi mkubwa wa maji wa Kemondo- Maruku unaogharimu Bilioni 15.8. Mradi huu umeshaanza kutoa huduma kwa wananchi wa Kata 3 za Tarafa ya Katerero ambazo ni Kemondo, Bujugo na baadhi ya maeneo ya Kata ya Katerero huku ukitarajia kunufaisha Kata 7 ukishakamilika wote kwa 100%.
