UWEKEZAJI WA MIUNDOMBINU MIZURI YA ELIMU IENDANE NA UTOAJI WA ELIMU BORA


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za  Mitaa(TAMISEMI)imeishauri Ofisi ya Rais - TAMISEMI  kujenga, kusimamia na kufuatilia utekelezwaji wa ujenzi wa miradi ya elimu ihakikishe ujenzi huo uendane  sambamba na utoaji wa elimu bora.

Kauli hiyo imetolewa   Oktoba 28, 2023 wakati  kwenye ziara yenye lengo la kukagua miradi ya elimu  inayotekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Nyamagana Mkoani Mwanza.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati Makamu Mwenyekiti Mhe.Justin Nyamoga amesema Serikali imewekeza fedha nyingi katika elimu na inaendelea kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu  hivyo ni vyema  walimu wakajikita katika utoaji wa elimu bora nchini.

Amesema pamoja na uwekezaji huo  Wizara ya TAMISEMI pamoja na mipango yake mengine lakini pia iendelee kuongeza  miundombinu ya kufundishia na kujifunzia kwa  walimu pamoja  na vifaa vya kufundishia. 

Kamati ikatoa maelekezo kwa uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuhakikisha wanasimamia na  kushughulikia eneo linalotarajiwa kujengwa kituo cha mafuta karibu na shule hiyo ili eneo hilo libaki kuwa la  shule kwa ajili ya usalama.

Kwa upande wa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais -TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi amesema utekelezaji wa miradi hiyo ni usimamizi madhubuti wa uongozi unaongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluh Hassan  kwa kuitekeleza Ilani ya CCM kwa kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi wote.

Amesema miradi  hiyo inatekelezwa nchi nzima na  Mhe. Rais ametoa zaidi ya tshs. Bil.7.9 kuboresha elimu ya Sekondari na zaidi Bil.12 kuboresha elimu ya Awali na  msingi.

Post a Comment

Previous Post Next Post