MAWAZIRI BASHUNGWA NA MWIGULU WAWASILI MBEYA KWA ZIARA YA KIKAZI


Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) pamoja na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), wamewasili  mkoani Mbeya kwa ziara ya kikazi, leo Oktoba 01, 2023. 


Mawaziri hao wamepokelewa na Mkuu wa Mkoa Mbeya, Mhe. Juma Homera katika ofisi yake na wataendelea na ziara katika wilaya ya Busokelo. 


Katika ziara hiyo, watakagua mradi wa barabara ya  Katumba - Mbambo- Tukuyu; Lot 3: Katumba - Lupaso (Kilometa 35.3) na Mbaka- Kibanja (Kilometa 20.7) pamoja na kufanya mkutano wa kuzungumza na wananchi Kandete mjini. 

Post a Comment

Previous Post Next Post