MISS WORLD TANZANIA 2026 WAAPA KUIBRAND SGR NCHINI VIETNAM


Walimbwende 20 wanaoshiriki kinyang'anyiro  cha  kumsaka mnyange  wa  Tanzania ( Miss Tanzania) atakae wakilisha nchi katika mashindano ya ulimbwende duniani,  yanayotarajiwa kufanyika nchini Vietnam kati ya Agosti na Septemba, 2026 wameahidi kuipeperusha SGR duniani kupitia mashindano hayo.

Walimbwende hao wametoa kauli hiyo Machi 13, 2026 waliposafiri  na SGR kati ya Dar Es Salaam  Dodoma kwa kutumia SGR, kwa lengo la kujifunza na kuongeza upeo.

Mkurugenzi wa kitaifa wa Shindano hilo Mustafa Hassanali, akizungumza mara baada ya kuwasili Dodoma, pamoja na mambo mengine amesema, walimbwende hao wameamua  kutumia usafiri wa SGR kwakuwa wamelenga kupitia Miss World, kuiambia dunia kuwa Tanzania haina  uzuri wa asili pekee , bali pia miundombinu ya kisasa na salama.

"Miss World ni jukwaa la kimataifa la kuibrand nchi  husika, mashindano haya yana washiriki kutoka zaidi ya nchi 100 na huangaliwa na mamilioni ya watu duniani. Kufuatia hilo nchi zinazoshiriki hutumia fursa hii kuonyesha, mambo kadhaa kama utamaduni vivutio vya utalii,maendeleo ya kiuchumi na miundombinu" amemalizia Hassanali.

Katika hatua nyingine,  baadhi ya walimbwende wanaoshiriki mashindano hayo wameeleza kufurahishwa kwao na  usafiri wa SGR na kuahidi kuinadi  nchini Vietnam ambako mashindano ya dunia yatafanyika kati ya  Agosti na  Septemba, 2026.

Silya Mussa mshiriki wa Miss World Tanzania ameipongeza serikali kwa ujenzi wa SGR ambayo imechochea kukua kwa sekta mbalimbali ikiwemo utalii  na kama kijana ameahaidi kuinadi reli ya SGR   katika Mashindano  nchini Vietnam.

Kwa upande wake,Christina Mbaga, amesema endapo atafanikiwa kutwaa taji la Miss World Tanzania ameahidi kuinadi SGR kama ilivyo kwa  vivutio vingine ikiwemo mbuga za wanyama, mito na madini.

Huduma za SGR zimekuwa chachu kubwa  katika kuchagiza uukuaji wa kisekta  nchini hivyo ni jukumu la Watanzania kuitangaza Sekta hii.

Post a Comment

Previous Post Next Post