MAHAWANGA AWATAKA MABINTI NA VIJANA KUTUMIA VIPAJI VYAO KAMA FURSA YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Mbunge  wa  Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tisha Mama Foundation Mhe. Mahawanga Janeth, amezindua Program ya Sanaa ya Uchoraji  kwa Mabinti na Vijana katika Kituo cha Don Bosco, Upanga Mkoani  Dar es Salaam. 

Katika Uzinduzi  huo Viongozi mbalimbali walihudhuria wakiwemo Wah. Madiwani wa Viti Maalumu  kutukoka  Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni, Diwani kata ya Mbezi Juu, Meneja wa Miradi wa CRDB  Bank Ndg. Baraka Kiyalo, Viongozi wa
Serikali  za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu sambamba  na wadau mbalimbali  wa masuala ya uwezeshaji  wanawake  kiuchumi na Vijana.

Mhe. Mahawanga  amewataka  Mabinti na Vijana wote wenye vipaji  na mawazo ya maendelo katika Mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza kwani Taasisi ya Tisha Mama Foundation itawasaidia kugeuza Vipaji na Mawazo yao kuwa fursa lakini pia amewaahidi kuwa nao bega bega kuwasaidia mpaka kufikia lengo kubwa la kuhakikisha  vijana na Wanawake wanajikomboa kiuchumi kupitia fursa zinazopatikana ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha Mhe. Mahawanga ameeleza namna ambavyo Taasisi ya Tisha Mama Foundation ilivyoona kipaji cha pekee  cha Uchoraji cha Binti Mhellepu Shillingi na kumpa Tuzo ambapo sasa amekuwa Mwalimu na sehemu ya Mabinti wengine ambao wameanza kupatiwa mafunzo  ya uchoraji na kufikia katika hatua nzuri mpaka kufika mwakani 2024 mwezi wa nne watakuwa wamehitimu nao watakwenda kuwa chachu ya kuwasaidia Mabinti wenzao na vijana kiujumla.

Mhe. Mahawanga amepongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt Samia Suluhu  Hassan  kwa namna ambavyo amekuwa akiwezesha makundi mbalimbali  ya Vijana  na Wanawake  kiuchumi  na kuahidi hatokuwa nyuma katika hilo kwa kumuunga mkono Rais Dkt Samia kupitia Taasisi  yake na Ofisi ya Mbunge kutoa fursa hizo kwani umekuwa ni mchango mkubwa kwa kuhakikisha  kituo hicho cha  Mafunzo cha Mabinti na Vijana kwenye Uchoraji  kinasimama imara na kinakwenda kuleta tija kubwa kwa kuibua Vipaji kwa wengine.

Aidha Meneja  Miradi wa CRDB, Ndugu. Baraka Kiyalo, amepongeza jitihada za  Tisha Mama Foundation katika kusaidia jamii hasa Mabinti, Vijana wa kiume na Wanawake na kusema benki hiyo ipo  tayari kusaidia jamii  kupitia taasisi hiyo  kufanikisha  ndoto zao  na kuwafanya kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo  ikiwemo mikopo isiyo na riba ya Imbeju.

Nao Madiwani wa Viti Maalumu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, wameipongeza Tisha Mama Foundation hususan Mbunge Mahawnga kwa jitihada  kubwa zinazofanyika kuwasogeza karibu na fursa na kuwataka wasichana hao walioanza kupata mafunzo hayo kueneza fursa hiyo kwa wenzao wengine na kuahidi kushirikiana  na Mbunge Mhe. Mahawanga sambamba  na Taasisi ya Tisha Mama Foundation kwenye  maeneo  yao kuibua vipaji mbalimbali vya Mabinti na Vijana na kuangalia namna bora ya kuwawezesha.

Pia Mkufunzi wa Uchoraji Bi. Mhellepu, ameishukuru Tisha Mama Foundation kwa kuwawezesha kimafunzo na kwamba dhamira yao  ni kuwa wachoraji wakubwa wa Kimataifa na kutumia vipaji vyao  kuwa fursa ya ajira ambapo pia Mkuu wa Don Bosco Upanga, Father  Peter Mkechura, alisema kituo hicho kinaishukuru Tisha Mama Foundation  kwa kuwa mdau muhimu kusaidia Mabinti hao kutimiza ndoto zao  na kuomba jamii kusaidia watoto wenye Vipaji  kuonyesha taranta walizonazo.

Post a Comment

Previous Post Next Post